
Mwenyekiti
Wa Uvccm Taifa Ndugu Kheri James, Amewaomba Radhi Watanzania kwa niaba ya Uvccm
ikiwa waliwahi kukwazwa au kukosewa kwa namna moja ama nyingine na maneno ama
matendo ya Uvccm.
Akiongea
na vyombo vya habari, Jumapili 28, march 2021 Jijini Dodoma, Kheri James
alinukuliwa akisema "Kama kuna jambo huko nyuma ambalo kwa maneno ama matendo
ambalo litatumika kama rejea ya kuzuia hiyo dhamira ya Rais wetu, sisi tunasema
tunaomba radhi na tuko tayari kushirikiana na Rais wetu ili kuhakikisha dhamira
yake haikwazwi na matendo wala maneno yetu.’’
Kauli
hiyo imekuja siku chache baada ya mazishi ya aliekuwa Rais wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dr.John pombe Magufuli aliyekuwepo madarakani.
Aidha
ndugu Kheri james amaeongeza kuwa vijana wanapaswa kuwa kielelezo cha maendeleo
ya nchi na kuwa mstali wa mbele kumuunga mkono Rais mpya wa Jamhuri ya muungano
wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan “Jukumu letu la msingi tunalotakiwa
kulifanya kama vijana ni kuhakikisha hii dhamira njema aliyonayo Rais wetu
kuhusu umoja wa watanzania, haki zao, usawa wao pamoja na mwelekeo wao kama
taifa sisi tunakuwa ndio nguzo imara kuhakikisha haya yanatokea, tusiende
tukachochea uadui, chuki, na uhasama na ikiwa yaliwahi kufanyika, sisi tuna
haki na wajibu wa kuombana radhi na kuanza upya kama taifa.” Kheri james.
Taarifa hiyo imepokelewa kwa ukosolewaji mkubwa kutoka kwa jamii, ikidaiwa haijaonesha kukiri moja kwa moja makosa ambayo wengi waliyaona huko nyuma, kipindi cha serikali iliyopita.
👉Aombe radhi yeye binafsi tafadhari na kinagaubaka akiainisha hilo alilolinena. 🎺Na si kwake tu bali woote walioeneza chuki kila mmoja achukue hii fursa ya kuomba radhi.
— chawamkuu (@chawamkuu) March 29, 2021
🎷Lakini hii ya kiujumla tena eti kwa kauli kuwa "kama sijui tulikosea..." Ni upumbavu.
✍️Simama uhesabiwe
Mimi mkatoliki, na nimefundishwa ukitaka usamehewe dhambi zako unaenda mbele za Mungu Ukiongozwa na Padri, Unataja Dhambi kama Ulivo itenda Mfano Nilizini, Niliua, Nilitamani nk afu unaomba Usamehewe. Sasa Ndugu yetu Erick Ngambeki aka Heri james Tumsamehe kwa Dahambi zipi???
— Vitus Nkuna (@VitusNkuna) March 29, 2021
Leave a comment