
Twitter
imetangaza kufungia kabisa akaunti yake ya twitter @realDonaldTrump, na akaunti
ya kampeni ya @TeamTrump kutokana hatari ya kuchochea vurugu zaidi kufuatia
vurugu zilizojitokeza katika jumba la Capitol Hill.
Twitter
imetoa hiyo taarifa usiku wa kuamkia leo na kuongeza kuwa awali ilifunga
akaunti ya Rais huyo kwa kuwa ilikuwa inaonekana kuchochea ghasia zaidi.
"Baada
ya kuchunguza kwa karibu jumbe zinazochapishwa kwenye akaunti ya
@realDonaldTrump na muktadha unaozunguka jumbe hizo na namna zinavyotafsiriwa
ndani na nje ya Twitter - tumesimamisha kabisa akaunti hiyo kwa sababu
zinaonekana kuhamasisha vurugu zaidi,”. kampuni hiyo aliandika katika chapisho
la blogi
"Katika
vurugu za kutisha zilizojitokeza hivi karibuni, tuliweka wazi Jumatano kwamba
ukiukaji zaidi wa taratibu za Twitter ungeweza kusababisha hatua hii,"
taarifa ilieleza.
Rais
Trump alifungiwa akaunti yake ya Twitter kwa saa 12 Jumatano baada ya kutoa wito
kwa wafuasi wake kuvamia bunge ambao aliwaita "wazalendo".
Mamia
ya wafuasi wake walivamia bunge wakijaribu kuvuruga kikao cha kuidhinisha
ushindi wa Bwana Biden kama Rais. Vurugu hizo zilisabaisha vifo vya raia wanne
na afisa mmoja wa polisi.
Mtandao
wa Twitter baadaye ukaonya kuwa unaweza kumpiga marufuku Bwana Trump kuutumia
kabisa ikiwa atakiuka tena kanuni za jukwaa hilo la mawasiliano.
Baada
ya akaunti yake ya Twitter kuwezeshwa tena, Bwana Trump alituma ujumbe kwenye
mtandao wa Twitter Ijumaa kuwa kampuni hiyo ilikuwa na mwisho kuchochea.
Katika
moja ya ujumbe wake aliandika: "Wamarekani 75,000,000 Wazalendo
walionipigia kura, Marekani Kwanza na Fanya Marekani kuwa Bora Tena, watakuwa
na sauti inayosikiza siku zijazo. Hawatakosewa heshima au kuchukuliwa kwa
uonevu kwa namna yoyote ile !!!"
Mtandao
wa Twitter umesema ujumbe huo "unatafsiriwa kama ishara zaidi ya kuwa Rais
Trump hana mpango wa kuhakikisha kunafanyika 'mabadilishano ya mamlaka kwa njia
ya amani'".
Hata
baada ya kufungiwa akaunti binafsi Trump hakuishia hapo alishiriki ujumbe
kupitia akaunti rasmi ya Rais wa Marekani @POTUS akisema kuwa "ataangalia
uwezekano wa kuwa na mtandao wao utakaowezesha mawasiliano siku za usoni"
na kukosoa Twitter. ingawa Twitter waliuondoa muda mfupi baada ya kuwekwa.
TRUMP
ANASEMA HATAHUDHURIA UZINDUZI WA BIDEN
Rais
Trump amesema kuwa hatohudhuria sherehe za kuapishwa rais wa 46 wa Marekani,
Joe Biden.
Mtandao
wa Twitter umesema kuwa ujumbe huo "umechukuliwa na wafuasi wake kadhaa
kama thibitisho la kwamba uchaguzi huo haukuwa halali".
Mtandao
wa Twitter umesema ujumbe wote huo alioandika "unakiuka sera na kanuni
katika uhamasishaji wa vurugu".
Hatua
hii itakuwa mara ya pili kwa Rais aliyepo madarakani kutohudhuria, ya kwanza
ikiwa 1869 ambapo Andrew Johnson alisusa baada ya kuondolewa madarakani na
Bunge la nchi hiyo.
Kwa kawaida, Rais aliyepo madarakani
hupanda gari moja na Rais anayeingia madarakani kuelekea eneo la uapisho, ikiwa
ni ishara ya umoja na kukabidhiana madaraka kwa amani na utulivu.
Leave a comment