
Twitter na Facebook zimechukua hatua ya kufungia akaunti za Rais Trump baada ya kutuma ujumbe kwa wafuasi wake waliovamia bunge
la Marekani
Twitter iliondoa jumbe tatu kutoka kwenye akaunti
ya Rais Donald Trump siku ya Jumatano na kusimamisha akaunti yake kwa masaa 12
baada ya Rais huyo kuendelea kushinikiza nadharia potofu kuhusu
uchaguzi pindi umati ulipovamia bunge la Marekani.
Kampuni hiyo pia ilionya kuwa ukiukaji zaidi
wa sheria zake "utasababisha kufutiliwa mbali" kwa akaunti ya Twitter
ya Rais Trump.
Moja ya jumbe ni pamoja na video ya Trump
akirudia madai yasiyo na msingi kwamba uchaguzi ulihujumiwa huku akiwahimiza
wafuasi wake kutawanyika baada ya ghasia kuzuka ndani na nje ya jumba la
Capitol Hill. Alisema kuwa sheria na utulivu zinahitajika akidai kwamba
anawapenda wafuasi wake.
Facebook na YouTube pia ziliondoa kanda ya
video kutoka kwenye akaunti ya Trump kwa sababu ilikiuka sera inayopingana na
kusambaza madai ya udanganyifu kuhusu uchaguzi uliopita. Facebook ilisema
ilizuia akaunti ya Rais huyo kwa masaa 24 kwa madai ya kuwa alikuwa anachochea
badala ya kupunguza ghasia zilizokuwa zikiendelea.
Hapo awali Twitter haikuwa imeondoa akaunti
ya kiongozi huyo badala yake iliondoa uwezo wake wa kujibiwa , kupendwa na
kutolewa maoni ikiwa nma ujumbe uliosomeka "Madai haya ya ulaghai wa
uchaguzi si halali, na chapisho hili haliwezi kujibiwa, kutolewa maoni,
au kupendwa kwa sababu linahatarisha hali ya usalama."
Twitter ilisema kupitia moja ya akaunti za kampuni
yake kwamba ikiwa Trump ataondoa machapisho yake, akaunti yake itafunguliwa.
Uondoaji huo ni hatua kubwa zinazofanywa na
kampuni hizo za mitandao ya kijamii tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali
ambapo walikuwa wanasita kuchunguza na kuchukua uamuzi juu ya machapisho
ya viongozi wakubwa wa kisiasa kama Rais. Twitter na Facebook wameweka mfumo za
kukagua ukweli kwenye baadhi ya machapisho ya Trump kuchunguza
walijumuisha habari ambazo zinakiuka sheria zao, na hapo awali Twitter
ilishawahi kufungia kwa muda akaunti binafsi na za kampeni za Rais Trump.
YouTube ilisema katika taarifa kwamba video hiyo
ilikiuka "sera kuhusu maudhui ambayo yanadai udanganyifu kuhusu
uchaguzi uliopita.”
Facebook ilisema: "Maandamano ya vurugu
huko Capitol leo ni aibu. Tunakataza uchochezi na wito wa vurugu kwenye jukwaa
letu. Tunakagua na kuondoa maudhui yote yanayokiuka sheria hizi."
Makamu wa Rais wa Uadilifu Facebook, Guy Rosen alichapisha ujumbe uliosomeka ”Hii ni hali ya dharura na tunachukua hatua zinazostahiki ikiwa ni pamoja na kuondoa video ya Rais Trump. Tumeiondoa kwa sababu tunaamini inachangia badala ya kupunguza hatari ya vurugu zinazoendelea ."
Leave a comment