
Mgogoro kati ya Shirika la Utangazaji nchini Tanzania
na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umemalizika baada ya viongozi
wakuu wa aasisi hizo kukutana na kujadili suala hilo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jukwaa la Wahariri
nchini Tanzania kupitia kwa Katibu wa Jukwaa hilo Nivville Meena, imesema kuwa
kikao hicho cha maridhiano kilichofanyika katika ofisi za makao makuu ya Tume
ya Uchaguzi NEC, yaliyopo mkoani Dodoma
kilihusisha viongozi wa taasisi tatu ambao ni pamoja na Kaimu Mwenyekiti
wa Jukwaa la Wahariri Deodatus Balile, Mkurugenzi wa TBC Ayubu Ryoba,
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe pamoja
na Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Dkt Willson Mahella Charles.
Mkurugenzi wa shirika la Utangazaji TBC, Ayubu Ryoba
amesema kuwa hatua iliyochukuliwa na CHADEMA ya kuwafukuza waandishi wa habari
wa chombo hicho katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni wa chama hicho
uliofanyika katika uwanja wa Zakiem, Mbagala Jijini Dar es Salaam ililenga
kubomoa kiwango cha TBC kuaminika kwa umma, na pia kukiri makosa yaliyofanywa
na watangazaji wa kituo hicho wakati wakirusha matangazo hayo na kuahidi kuwa
shirika halitarudia makossa yaliyojitokeza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe
ameeleza kuwa uhusiano kati ya chama hicho na TBC umekuwa si mzuri kwa muda
mrefu, na kwamba hata vyombo vingine vya habari vimekuwa vikikataa kurusha
matangazo yao hata kama kimelipia kwa maelezo ya kuwa kimepewa maelekezo kutoka
juu. Freeman Mbowe amevitaka vyombo vya habari kufaya kazi kwa weledi katika
kipindi chote cha kampeni
Awali Mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi wakati akifungua
kikao hicho alieleza kuhusu umuhimu wa vyombo vya habari vya umma na wajibu
wake katika kutoa fursa kwa vyama vyote vya siasa kwa mujibu wa sheria. Lakini
pia mwenyekiti wa Baraza la Wahariri, Deodatus Balile, ameeleza umuhimu wa
vyombo vya habari kushirikiana na vyma vya siasa pamoja na vyama vya siasa
kushirikiana na vyombo vya habari hasa katika kipindi cha kampeni
Baada ya mjadala katika ya pande zote mbili Mkurugenzi
wa Shirika la Utangazaji Tanzania, TBC, Ayub Ryoba pamoja na Mwenyekiti wa
CHADEMA Freeman Mbowe walikubaliana kumaliza tofauti zao na kurejesha
ushirikiano ambapo Mbowe amesema kuwa atawatangazia wanachama wa CHADEMA kuwa
wapo tayari kufanya kazi na TBC, na TBC wameiomba CHADEMA kuwapa ratiba yao ya kampeni
ili waweze kuendelea kurusha matangazo yao.
Leave a comment