
Marekani imetangaza kuwawekea vikwazo vya kuingia nchini humo maafisa wa Tanzania ambao nchi hiyo inawatuhumu kwa kile wanachokitaja kuwa kuingilia uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka 2020.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo, Waangalizi wa uchaguzi na mashirika ya kiraia wanadai kuwepo kwa udanganyifu katika uchaguzi huo pamoja na uvunjifu wa haki za binadamu wakati na baada ya uchaguzi.
There are consequences for interfering in the democratic process. Starting today, we are imposing visa restrictions on those involved in election interference in Tanzania. We remain committed to working together to advance democracy and mutual prosperity for both our countries.
— Secretary Pompeo (@SecPompeo) January 19, 2021
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Marekani itaendelea kufuatia kwa ukaribu mwenendo wa mambo nchini Tanzania na haitasita kuwachukulia hatua wale wote inaodai kuwa wanaminya demokrasia na haki za binadamu.
Taarifa hiyo inakuja siku moja kabla ya utawala wa Rais anayemaliza muda wake, Donald Trump, kumalizika, ikiacha wasiwasi ikiwa utawala mpya wa Joe Biden utatekeleza hatua hiyo. Katika hali inayoonesha msuguano dhahiri baina ya viongozi hao wawili, ofisi ya Biden imesema kuwa itatengua sera kadhaa za Trump mara tu baada ya kuingia ofisini.
Utawala
wa Trump utakumbukwa kwa kuwekea vikwazo vya usafiri mataifa ya Afrika pamoja
na baadhi ya viongozi wa mataifa ya Afrika, akiwamo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam, Paul Makonda, kwa kile Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani
ilichokiita "kuwalenga watu waliotengwa katika jamii wakiwemo mashoga,
kuukandamiza upinzani pamoja na uhuru wa kujieleza."
Leave a comment