
Boeing italipa faini ya Dola bilioni 2.5 ambayo ni
takriban Tsh. Trilioni 5.7 kwa kosa la kuficha Taarifa za Kiusalama za Ndege za
737 Max ambayo ilipata ajali na kuua watu 346. Kampuni ya anga ya Boeing
imetozwa faini ya Dola za Kimarekani bilioni 2.5 ambayo ni takribani Tsh.
Trilioni 5.7 kufuatia ajali mbili zilisababishwa na ndege hizo.
Wizara ya sheria ya Marekani imesema ufumbuzi uliofikiwa unahusu adhabu
ya faini ya dola milioni 243.6, malipo ya dola bilioni 1.77 kwa wateja wa
kampuni ya Boeing 737 na kuanzisha mfuko wa dola milioni 500 kwa ajili ya fidia
kwa warithi, ndugu na jamaa wa watu waliokufa katika ajali.Ajali mbili za ndege
za Boeing 737 zilitokea nchini Indonesia mnamo mwaka 2018 na
nchini Ethipia
mnamo mwaka 2019 ambapo kwa jumla watu 346 walikufa.
Ajali
mbili za ndege za Boeing 737 Max zilizotokea nchini Indonesia mnamo 2018 na
nchini Ethiopia mnamo 2019 ambapo kwa ujumla idadi ya watu wakiwepo
wafanyakazi waliokuwa ndani waliaga dunia.
Baada
ya ajali hatua stahiki zilichukuliwa zikihusisha uchunguzi kadhaa ulioigharimu
kampuni hiyo karibu Dola za Kimarekani bilioni 20 .Safari za Ndege zote
za 737 Max zilisitishwa mpaka pale serikali ya Marekani ilipotoa ruhusa
kwa Boeing kuanza kuzirusha tena mnamo Novemba ambapo ndege
zilianza safari zake rasmi pindi ilipotimu Disemba mwaka jana.
Boeing ilihitajika kuboresha programu, mifumo na mafunzo yake kabla ya kubeba
abiria kwenye ndege.
Mkurugenzi
wa mamlaka ya anga nchini Marekani (US Federal Aviation Administration (FAA)
Chief), Steve Dickson alisema mwaka jana idara hiyo "imefanya kila
linalowezekana” kuhakikisha aina hizi za ajali hazitokei tena. Alisema alikuwa
na imani kwa asilimia 100 katika usalama wa ndege hiyo.
Taarifa
zilizofichwa zilikuwa ni kuhusu kubadili Mfumo wa MCAS ambao ulifanya Rubani
akose baadhi ya taarifa kuhusu Mfumo huo wa Uendeshaji ambapo walikuwa
wakilazimisha vinginevyo kwa kutojua.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni ya Boeing, David Calhoun alisema katika makubaliano hayo
"yanakubali kwamba walienda kinyume na maadili na matarajio".
Leave a comment